Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Society & Culture
Business
TV & Film
Sports
Health & Fitness
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts211/v4/95/60/cd/9560cdde-9c7f-d479-0f94-fa6c6ef9e8a7/mza_8923711405139386944.jpg/600x600bb.jpg
TANAPA PODCAST
Tanzania National Parks (TANAPA)
14 episodes
3 days ago
Karibu katika Podcast rasmi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), inayoangazia mazungumzo ya kina kuhusu Uhifadhi wa Maliasili zilizopo ndani ya Hifadhi za Taifa, Elimu ya Uhifadhi, Utalii pamoja na Fursa za Uwekezaji. Vipindi vya Podcast hii vinajadili mikakati ya uhifadhi endelevu, ukuaji wa utalii, na ushirikiano na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuhakikisha Rasilimali za Taifa zinatunzwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Show more...
Government
RSS
All content for TANAPA PODCAST is the property of Tanzania National Parks (TANAPA) and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.
Karibu katika Podcast rasmi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), inayoangazia mazungumzo ya kina kuhusu Uhifadhi wa Maliasili zilizopo ndani ya Hifadhi za Taifa, Elimu ya Uhifadhi, Utalii pamoja na Fursa za Uwekezaji. Vipindi vya Podcast hii vinajadili mikakati ya uhifadhi endelevu, ukuaji wa utalii, na ushirikiano na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuhakikisha Rasilimali za Taifa zinatunzwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Show more...
Government
Episodes (14/14)
TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 14: MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.

Episodi hii inaangazia mila, desturi na tamaduni katika uhifadhi wa maliasili, hususan namna jamii ya Wangoni kutoka mkoani Ruvuma ilivyotumia majina na utamaduni wao kulinda Wanyamapori na Misitu  tangu enzi za mababu zetu.

Hadithi hii ya kuvutia inaonesha jinsi urithi wa jadi ulivyokuwa chachu ya kulinda rasilimali za Taifa ambazo leo hii zinachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya uhifadhi na utalii.

Sikiliza simulizi hii adhimu kutoka kwa Chifu Songea Mbano wa Kwanza, kupitia TANAPA Podcast – Episode ya 14.


 Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena
Mgeni: Samweli Vitus Mbano (Chifu Songea Mbano I)


Usikose kila Jumatatu na Alhamisi kupitia majukwaa mbalimbali ya TANAPA Podcast

Show more...
3 weeks ago
55 minutes 20 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 13 - Mila na Tamaduni zilizohusisha mizimu katika kuhifadhi Maliasili

Episodi hii inakuletea mazungumzo ya kina kuhusu mila, tamaduni na makatazo ya Kabila la Wagongwe lililopo mkoani Katavi na jinsi taratibu hizo zilivyochangia kulinda maliasili na vyanzo vya maji. Mathalani; ilikuwa hairuhusiwi kukata miti iliyokuwa katika vyanzo vya maji kutokaana na imani ya kuwepo kwa nyoka mkubwa wala kuua mnyamapori hadi upewe kibali na pepo au jini Katabi anayepatikana katika Hifadhi ya Taifa Katavi. Sikiliza simulizi hii ya kuvutia katika epsodi ya 13.Eneo: Hifadhi ya Taifa KataviMwongoza kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena Wageni:1.⁠ ⁠Moses Edward Tende ( Mtemi Sigulu) Chifu wa Kabila la Wagongwe.2.⁠ ⁠Lukas Moses Msaga - Mtoto wa Mtemi Sigulu anayefundishwa kurithi mikoba ya Mtemi Sigulu.⁠3.⁠ ⁠⁠Askari Uhifadhi Daraja la Pili - Kimori Shiwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ikolojia, Hifadhi ya Taifa Katavi. Endelea kutufuatilia kupitia Platifomu za TANAPA Podcast.TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

Show more...
4 weeks ago
54 minutes 47 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 12 - Zoezi la Uhamishaji Tembo kutoka Misenyi kwenda Hifadhi ya Taifa Burigi - Chato.

Episodi hii imeangazia zoezi endelevu la kuwahamisha tembo walowezi kutoka maeneo ya karibu na wananchi kwenda hifadhini na zoezi zima la kuwaswaga tembo waliotoka hifadhini kuvamia maeneo ya wananchi na kuwarudisha hifadhini.


Sikiliza Episodi hii kwa taarifa hiyo na mengine mengi kupitia Epsode ya 12.


Eneo: Misenyi - Bukoba.


Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena


Guests: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Dkt. Fredrick Mofulu - Mkuu wa Hifadhi Ibanda - Kyerwa.

Na

Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Charles Ngendo - Mkuu wa Hifadhi Rumanyika - Karagwe.


Fuatilia kupitia Platform za TANAPA Podcast.

Show more...
1 month ago
50 minutes 2 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 11 - Nyumba ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere na Historia ya Taifa letu.

Kuelekea Kumbukizi ya Kifo cha Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere Oktoba 14, TANAPA PODCAST tunakueletea uchambuzi kuhusu historia ya harakati za uhuru wa Tanganyika zilizoongozwa na Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Hapa utapata kujifunza mengi kuhusu harakati za Uhuru wa Tanganyika na Afrika kwa ujumla.


Ikumbukwe historia hii imehifadhiwa katika Nyumba ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere iliyopo Magomeni Usalama jijini Dar es Salaam. 

Fuatilia uhondo huo katika Epsode ya 11.


Eneo: Dar es salaam


Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena

Guest: Afisa Mhifadhi Mkuu Mariam Njaritha - Mkuu wa Kituo Nyumba Kumbukizi ya Mwl. Nyerere


Usikose kila Jumatatu na Alhamisi kupitia Platform za TANAPA Podcast.

TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

Show more...
1 month ago
41 minutes 52 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 10 - MAANDALIZI YA TWENZETU KILELENI 2025 NA PROF. KAMUZORA

Episodi hii inaangazia mazungumzo ya kina kuhusu zoezi la upandaji wa Mlima Kilimanjaro ambapo Profesa Kamuzora anaeleza uzoefu wake katika kupanda mlima kwa muda mrefu.


Fahamu faida ya kushiriki kampeni ya “Twenzetu Kileleni katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa Taifa letu, kuhamasisha utalii pamoja na utunzaji wa mazingira.


Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena - Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano - TANAPA

Guest: Prof. Faustin Kamuzora - Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi UTT AMIS.


Show more...
1 month ago
44 minutes 52 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 09 - YAFAHAMU MAENEO YA MALIKALE YALIYOKASIMISHWA TANAPA
Episodi hii inaangazia maeneo ya Malikale yanayosimamiwa na TANAPA na faida zake. Maeneo hayo yamebeba historia za kale, biashara ya utumwa, utawala wa machifu, ukoloni na uhuru wa Taifa letu. Sikiiiza TANAPA PODCAST Epsode 09 upate elimu ya kina kuhusu historia ya Taifa letu, asili na umuhimu wa kutunza tamaduni zetu. Eneo: Dar es Salaam. Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena. Guest: Afisa Uhifadhi Mkuu Malikale, Neema Mbwana.
Show more...
1 month ago
56 minutes 6 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 08 - MAANDALIZI YA TWENZETU KILELENI 2025 NA CDF (Mst.) GEORGE WAITARA


Katika Episode hii tunaangaIa mazungumzo ya kuhusu Kampeni ya Twenzetu Kileleni 2015 inayofanyikaga Desemba 09 kila mwaka kukumbuka mashujaa wetu waliopigania uhuru wa Tanganyika ambapo kwa mwaka huo huo bendera ya Taifa ilipandishwa Mlima Kilimanjaro wenye kilele kirefu kuliko vyote Barani Afrika chenye urefu wa mita “5985 asl” kuangazia nuru ya Uhuru ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.


Sikiliza TANAPA PODCAST Epsode 08 kwa habari za kweli na uhakika kuhusiana na historia ya Taifa letu, Uhifadhi na Utalii.


Eneo: Dar es Salaam.


Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena

Guest: Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Marwa Waitara.

Show more...
1 month ago
40 minutes 22 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 07 - Uchambuzi wa maneno yenye mkanganyiko katika Sekta ya Uhifadhi na Utalii

Episodi hii inaangazia uchambuzi wa kina kuhusu maneno mbalimbali yanayoleta mkanganyiko wa maana na matumizi yake katika jamii.

Katika Episode 07 Mtopezi wa lugha ya Kiswahili kutoka Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) Ndugu Oni Sigala anachambua na 

kudadavua maneno kadha wa kadha yenye utata katika sekta ya uhifadhi na utalii.


Eneo: Dar es salaam


Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena

Mgeni: Oni Sigala - Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA)


Usikose kila Jumatatu kupitia Platifomu za TANAPA Podcast.

Show more...
1 month ago
43 minutes 56 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 06 - Mila, Desturi na Tamaduni katika Uhifadhi wa Maliasili

Sikiliza Episode 06 uchambuzi wa kina katika mwendelezo wa mada inayoeleza elima ya Uhifadhi ikihusisha Mila, Desturi, Tamaduni na Miiko iliyozuia uharibifu wa Maliasili za Taifa ambapo moja ya maeneo hayo kwa sasa ni Hifadhi za Taifa


Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena

Guest: Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara, Massana Mwishawa.

Show more...
1 month ago
37 minutes 21 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 05 - Mila, Desturi na Tamaduni katika Uhifadhi wa Maliasili

TANAPA Podcast Episode 05 inaangazia mwendelezo wa mada inayoeleza elimu ya Uhifadhi iliyohusisha Mila, Tamaduni, Desturi na Miiko anuwai iliyozuia baadhi ya wanyamapori kuuwawa lengo likiwa ni kuhifadhi maliasili zilizokuwa ndani ya maeneo yaliyohifadhiwa ambayo baadhi yake kwa sasa ndio Hifadhi za Taifa tunazozishuhudia zikitiririsha nyomi ya watalii nchini.


Eneo: Hifadhi ya Taifa Serengeti


Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena

Wageni: Barnabas Murigo, Kenyatta, Musoka na Stanslaus Mayani


Usikose kila Jumatatu saa 11:00 jioni kupitia TANAPA Podcast.


TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

Show more...
2 months ago
1 hour 33 minutes 52 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 04 Mila, Desturi na Tamaduni zilizotumika katika Uhifadhi wa Maliasili

Episode hii inaangazia mazungumzo katika ya Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TANAPA, Catherine Mbena na Mzee Fanuel Mbise, Eliona Miley na Elikesia Akyoo kuhusu elimu ya Uhifadhi kupitia mila, desturi na tamaduni zilizotumika katika kusheshimu na kutunza maliasili zilizokuwa zimehifadhiwa.

Show more...
2 months ago
57 minutes 35 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 03 Chimbuko la Uhifadhi

Sikiliza TANAPA Podcast, Episode 03 uelimike kuhusu

Chimbuko la Uhifadhi

Uanzishaji wa Hifadhi mpya na malengo yake

Maeneo matano ya Malikale yaliyokasimishwa TANAPA na

Uzalendo katika kutembelea Hifadhi za Taifa.


Mgeni maalum: Nakaaya Sumari (Tanzania Safari Channel)

Host: ACC Catherine Mbena, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano TANAPA


Fuatilia mfululizo huu wa elimu ya uhifadhi, utalii na mirindimo iliyojaa burudani na maarifa tele.

Show more...
2 months ago
43 minutes 7 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 02 - Kazi mbalimbali zinazofanywa na TANAPA

Katika episode ya pili ya mfululizo huu, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TANAPA, Catherine Mbena anaelezea kwa kina kazi mbalimbali zinazofanywa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika kuhakikisha maliasili zilizopo ndani ya hifadhi za Taifa zinaendelea kulindwa na kuhifadhiwa kwa faida ya kizazi hiki na vizazi vijavyo.

Show more...
3 months ago
19 minutes 18 seconds

TANAPA PODCAST
TANAPA PODCAST EPISODE 01 Utangulizi kuhusu TANAPA na majukumu yake

Katika episode hii ya kwanza, tunazungumzia kwa kina kuhusu Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) – kuanzia majukumu yake makuu, muundo wa utendaji kazi, hadi maeneo ya hifadhi yanayosimamiwa chini ya sheria. Ni programu endelevu inayokufahamisha nafasi muhimu ya TANAPA katika kulinda maliasili na kukuza mapato yatokanayo na shughuli za utalii.



Show more...
3 months ago
17 minutes 49 seconds

TANAPA PODCAST
Karibu katika Podcast rasmi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), inayoangazia mazungumzo ya kina kuhusu Uhifadhi wa Maliasili zilizopo ndani ya Hifadhi za Taifa, Elimu ya Uhifadhi, Utalii pamoja na Fursa za Uwekezaji. Vipindi vya Podcast hii vinajadili mikakati ya uhifadhi endelevu, ukuaji wa utalii, na ushirikiano na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuhakikisha Rasilimali za Taifa zinatunzwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.