
Episodi hii inaangazia mila, desturi na tamaduni katika uhifadhi wa maliasili, hususan namna jamii ya Wangoni kutoka mkoani Ruvuma ilivyotumia majina na utamaduni wao kulinda Wanyamapori na Misitu tangu enzi za mababu zetu.
Hadithi hii ya kuvutia inaonesha jinsi urithi wa jadi ulivyokuwa chachu ya kulinda rasilimali za Taifa ambazo leo hii zinachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya uhifadhi na utalii.
Sikiliza simulizi hii adhimu kutoka kwa Chifu Songea Mbano wa Kwanza, kupitia TANAPA Podcast – Episode ya 14.
Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena
Mgeni: Samweli Vitus Mbano (Chifu Songea Mbano I)
Usikose kila Jumatatu na Alhamisi kupitia majukwaa mbalimbali ya TANAPA Podcast