Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Society & Culture
Business
Sports
Health & Fitness
Technology
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
Loading...
0:00 / 0:00
Podjoint Logo
US
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts211/v4/c5/3e/cc/c53ecc68-397d-991d-b35b-5016ab775c75/mza_1256632132512185068.jpg/600x600bb.jpg
Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
RFI Kiswahili
24 episodes
4 days ago

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.

Show more...
News
RSS
All content for Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii is the property of RFI Kiswahili and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.

Show more...
News
Episodes (20/24)
Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Rais W.Ruto amtunuku hayati Raila Odinga, nishani ya juu zaidi, hali mashariki ya DRC
Hatua ya rais wa Kenya William Ruto kumtunuku aliyewahi kuwa waziri Mkuu na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, hayati Raila Odinga, nishani ya juu zaidi nchini, kukamatwa kwa makamu mwenyekiti wa chama cha Chadema nchini Tanzania, John Heche, DRC na Rwanda zakubaliana juu ya mchakato wa upatikanaji wa amani chini ya upatanisho wa Marekani, uchaguzi wa urais nchini Cote D’Ivoire, na rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarcozy wiki hii alianza kukitumikia kifungo cha miaka mitano.
Show more...
1 week ago
20 minutes 3 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Kenya yaomboleza kifo cha RAILA, Jukwaa jipya la kisiasa DRC lazinduliwa
Miongoni mwa matukio makubwa yaliyojiri wiki hii ni pamoja na wakenya kuomboleza kifo cha mwanasiasa mashuhuri aliyewahi kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo Raila Amolo Odinga, kuzinduliwa kwa jukwaa jipya la kisiasa : Okoa DR Congo, kuendelea kwa kampeni za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu kule Tanzania, kuapishwa kwa kiongozi wa kijeshi wa Madagascar, na matukio mengine duniani.
Show more...
2 weeks ago
20 minutes 8 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Jeshi la Israeli kuondoka Gaza, rais wa DRC aitaka Rwanda kuchangia amani
Habari kuu wiki hii ni pamoja Israel kuanza kuwaondoa wanajeshi wake kwenye baadhi ya maeneo ya  Gaza, rais wa Ufaransa amteua tena Sebastien Lecornu kuwa waziri mkuu huku kukiwa na mvutano wa kisiasa, rais wa DRC, Félix Tshisekedi, amtaka mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame, kuwaamuru waasi wa M23 kuacha vita mashariki mwa Congo, siasa za kikanda, yaliyojiri huko Morocco, mwanaharakati wa demokrasia nchini Venezuela, Maria Corina Machado, ndiye mshindi wa tuzo ya amani ya Nobeli ya mwaka wa 2025
Show more...
3 weeks ago
20 minutes 7 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Hukumu ya kifo dhidi ya rais mstaafu wa DRC, kampeni za uchaguzi nchini Uganda
Kumekuwa na hisia mseto kuhusu hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya rais mstaafu wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Joseph Kabila, uzinduzi wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani nchini Uganda, hali ya nchini Tanzania wakati huu wananchi wakijiandaa kushiriki uchaguzi wa oktoba 29 mwaka huu, maandamano ya vijana Gen Z nchini Madagascar, na mashambulio ya mjini Manchester Uingereza.Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi 
Show more...
4 weeks ago
20 minutes 1 second

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Mkutano wa 80 wa Umoja wa mataifa, hali ya DRC na maandalizi ya uchaguzi Uganda
Baadhi ya habari ambazo tumezipa uzito ni pamoja na mkutano wa 80 wa baraza kuu la umoja wa mataifa wiki hii ambapo viongozi wa dunia walipata nafasi ya kutoa hotuba zao, kujiuzulu kwa spika wa bunge la DRC Vital Kamerhe, na kuendelea kwa mapigano mashariki mwa nchi hiyo, kuidhinishwa kwa wagombea wa kiti cha urais nchini Uganda kuelekea uchaguzi wa mwakani, Peter Mutharika kurejea madarakani baada kupata ushindi kwenye uchaguzi mkuu, kura ya maoni ya Guinea, na mambo mengine mengi.
Show more...
1 month ago
20 minutes 13 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Kesi ya rais mstaafu wa DRC kurejelewa, mbio za baiskeli kung'oa nanga huko Rwanda
Baadhi ya habari ambazo tumezipa uzito ni pamoja na vurugu katika bunge la DRC na mchakato wa kumuondoa spika wa bunge hilo na maafisa wengine, mashindano ya dunia ya baiskeli kung’oa nanga siku ya Jumapili mjini Kigali, mji mkuu wa Rwanda, siasa za Uganda kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani, tumeangazia hali nchini Tanzania, Sudan kusini, uchaguzi wa Malawi, kura ya maoni kule Guinea kuhusu marekebisho ya katiba na ziara wa Marekani huko Uingereza.
Show more...
1 month ago
20 minutes 9 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Zaidi ya watu 80 wafariki katika ajali ya boti Basankusu
Karibu kwa makala ya Yaliyojiri wiki hii. Baadhi ya habari ambazo tumezipa uzito wiki hii ni makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini ashatkiwa kwa uhaini na mauaji, ajali ya boti nchini DRC.
Show more...
1 month ago
19 minutes 46 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Hukumu dhidi ya waziri Mutamba nchini DRC, athari za misaada ya kigeni watoto wakizaliwa na HIV
Wiki hii taarifa zilizokuwa gumzo kwenye vyombo vya habari ni kuhusu hukumu dhidi ya aliyekuwa waziri wa sheria nchini DRC, Constant Mutamba, nitakujuza pia kuhusu kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania, tutaangalia pia ajali ya boti nchini Nigeria iliyoua watu 30. Kimataifa, tutaangazia punde zaidi katika mzozo wa Urusi na Ukraine.
Show more...
1 month ago
20 minutes

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Kampeni za uchaguzi wa Tanzania, mapigano DRC, Urusi yaendelea kuishambulia Ukraine
Kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu wa urais wa mwezi oktoba mwaka huu nchini Tanzania, kauli ya rais wa Rwanda Paul Kagame dhidi ya mzozo wa mashariki mwa DRC, mapigano makali kati ya jeshi la Congo FARDC na washirika wao wazalendo maeneo ya milima ya Fizi, hali nchini Sudan, ziara ya rais wa senegal jijini Paris ufaransa, Urusi yaendeleza mashambulio huko Kiev Ukraine licha ya shinikizo za Kimataifa na mengineyo.
Show more...
2 months ago
20 minutes 6 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Mkutano wa Trump na rais wa Ukraine na wakuu wa Ulaya, hali ya mashariki mwa DRC
Ni juma ambalo limeshuhudia mkutano kati ya rais wa Marekani Donald Trmp na rais wa Ukraine Volodmir Zelensky akisindikizwa na viongozi wa Ulaya, michuano ya CHAN kwenye nchi tatu za Afrika Mashariki yaendelea, mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu juma hili yalishutumu jeshi la Rwanda likishirikiana na waasi wa M23 kuwaua raia wa kawaida Binza wilayani Rutshuru mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, mkutano wa kimataifa wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Afrika au TICAD ulifunguliwa jijini Yokohama, Japani.
Show more...
2 months ago
20 minutes 6 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Mkutano wa uswis watamatika bila mkataba wowote, mapigano Ituri DRC yaua 31
Mkutano wa Geneva washindwa kupata mkataba wa kimataifa kuhusu taka za plastiki,  takriban watu 31 wakiwemo raia 19 waliuawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na wanamgambo wa CRP wa Thomas Lubanga katika eneo la Djugu mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa DRC, michuano ya CHAN 2024 kwenye nchi za Afrika Mashariki, hali ya Sudan, Somalia na mkutano wa rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin, huko Alaska.
Show more...
2 months ago
20 minutes 7 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Sintofahamu yaendelea kuhusu kuanza kwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Kinshasa na M23
Miongoni mwa taarifa utakazoziskia ni pamoja na; sintofahamu yaendelea kuhusu kuanza kwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Kinshasa na Muungano wa Vikosi vya Kidemokrasia vya Ukombozi wa Kongo AFC/M23, Rais wa DRC, Felix Tshisekedi amefanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri na kujumuisha upinzani.
Show more...
2 months ago
20 minutes 2 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Jumuiya za EAC na SADC kuujadili mzozo wa mashariki mwa DRC, hali ya Gaza
Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo juma hili zilifanya mkutano wa kwanza wa kamati ya pamoja ya usimamizi , kesi ya rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila ilisikilizwa kwa mara ya pili mjini Kinshasa, serikali ya Tanzania, ilipiga marufuku raia wa kigeni kufanya biashara ndogondogo, hali nchini Sudan kusini na Sudan, hatua ya rais wa Cote D’Ivoire kutangaza nia ya kuwania urais kwa muhula wa nne na kwengineko duniani.
Show more...
3 months ago
20 minutes 8 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Kesi ya rais mstaafu wa DRC J.Kabila yasikilizwa, mapigano kati ya Thailand na Kambodia
Kesi ya rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila ilifunguliwa mjini Kinshasa, waziri wa zamani wa sheria nchini DRC Constant Mutamba alikana mashtaka dhidi yake Kuhusu ubadhirifu wa fedha za umma, ripoti moja wiki hii ilisema Watu 65 waliuawa nchini Kenya kufuatia maandamano ya vurugu kati ya mwezi juni na julai, hali nchini Sudan kusini na Sudan lakini pia tutaangazia Afrika magharibi na mengine mengi
Show more...
3 months ago
20 minutes 9 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
DRC na waasi wa M23 kukubaliana kuhusu amani ya mashariki, Humphrey polepole akosoa CCM
Serikali ya Kinshasa na waasi wa AFC/M23 mbioni kusaini makubaliano ambayo kimsingi yanaleta matumaini ya kufikia amani mashariki mwa nchi hiyo, Tanzania yazindua dira ya maendeleo 2050 kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba, umoja wa mataifa wasema hali ya kibinadamu nchini Sudan si ya kuridhisha, rais Paul Biya, kiongozi mkongwe sana duniani na umri wa miaka 92 kuwania urais kwa muhula wa nane, umoja wa ulaya kutishia kuiwekea Urusi vikwazo vipya na hali ya nchini Syria
Show more...
3 months ago
20 minutes 11 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Rais Ruto aibua hisia kali kwa kuwaagiza polisi kuwapiga risasi ya miguu waandamanaji
Wiki hii watu wasiopungua 38 waliuawa nchini Kenya kufuatia maandamano ya SabasAba siku ya Jumatatu. Rais Ruto aliibua hisia kali alipowaagiza polisi kuwapiga risasi ya miguu waandamanaji.
Show more...
3 months ago
20 minutes 1 second

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Rais Kagame na Makubaliano ya Washington DC na mazishi ya Albert Ojwang Kenya
Yaliyoangaziwa katika makala hii ni pamoja na kauli ya rais wa Kenya kujenga kanisa ndani ya ikulu ya Nairobi, rais Paul Kagame wa Rwanda na mkataba wa amani ulioisainiwa kati ya nchi yake na DRC, waziri mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa kutogombea tena ubunge kuwakilisha jimbo la Ruangwa, hali nchini DRC, Sudan na kauli ya Ufaransa kuwa inatarajia Algeria kumsamehe mwandishi wa vitabu Boualem Sansal aliyefungwa, lakini pia mkutano wa viongozi wa Ulaya kule London Uingereza kufanyika wiki ijayo
Show more...
4 months ago
20 minutes 12 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Maandamano mapya yaua 16 Kenya, DRC na Rwanda zasaini makubaliano ya amani
Wiki hii ulimwengu umeshuhudia matukio mengi ya ajabu na hatari sana kwa usalama wa nchi mbali mbali, kwanza nchini Kenya watu 16 waliuawa katika maandamano ya kuadhimisha mwaka mmoja wa mauaji ya vijana Gen Z, Rwanda na DRC zatia saini mkataba wa amani kumaliza vita vya mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, siasa za Chad, Zambia na pia mashambulizi kati ya Israeli na Iran, pamoja na mkutano wa jumuia ya NATO..na mengine mengi
Show more...
4 months ago
20 minutes 13 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Israeli na Iran zaendelea kushambuliana, matukio mengine duniani
Mashambulio makubwa kwa makombora kati ya Israeli na Iran, na hali inayoendelea hadi sasa, maandamano ya kupinga kifo cha mwanablogu Albert Ojwang yaliyofanyika baada ya naibu Inspekta mkuu wa polisi Eliud Lagat kutangaza kujiuzulu nafasi kupisha uchunguzi, hali ya kisiasa nchini DRCbaada ya waziri wa sheria Constant Mutamba kujiuzulu, na vile vile siasa za ukanda wa Afrika mashariki, Afrika ya magharibi na kaskazini na kwengineko duniani.-
Show more...
4 months ago
20 minutes 1 second

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Mauaji ya mwanablogu nchini Kenya, Marekani yataka Jeshi la Rwanda kuondoka DRC
Mengi yamejiri nchini Kenya na maeneo mengine wiki hii lakini kubwa ni maandamano ya kupinga mauaji ya kijana Albert Ojwang na kutaka maafisa wa polisi waliohusika wajiuzulu, wiki hii Marekani iliitaka nchi jirani ya Rwanda kuwaondoa wanajeshi wake kwenye ardhi ya DRC kabla ya kusainiwa kwa mkataba wa Washington, pia utasikiliza mengine mengi kwengineko duniani
Show more...
4 months ago
20 minutes 12 seconds

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.