Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Business
Society & Culture
History
Sports
Health & Fitness
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts221/v4/de/da/12/deda1269-66cc-4374-f3a6-334feaca9f4d/mza_16441375759528457294.jpg/600x600bb.jpg
Wimbi la Siasa
RFI Kiswahili
24 episodes
21 hours ago

Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa

Show more...
News
RSS
All content for Wimbi la Siasa is the property of RFI Kiswahili and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.

Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa

Show more...
News
Episodes (20/24)
Wimbi la Siasa
Nini hatima ya Tanzania baada ya uchaguzi mkuu uliokumbwa na vurugu ?
Machafuko yalikumba uchaguzi mkuu wa Tanzania, uliofanyika Oktoba 29, 2025 na rais Samia Suluhu Hassan kutangazwa mshindi kwa kupata asilimia 97.6 ya kura. Chama kikuu cha upinzani CHADEMA, kimesema ushindi wa Samia ni kichekesho cha demokrasia. Anapaswa kufanya nini ili kuirejesha Tanzania katika utulivu wa kisiasa ? Tunachambua.
Show more...
1 day ago
10 minutes 16 seconds

Wimbi la Siasa
Watanzania wapiga kura bila uwepo wa upinzani
Watanzania wanapiga kura kuwachagua wabunge, madiwani na rais, katika uchaguzi ambao rais Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuibuka mshindi, baada ya mpinzani wake mkuu Tundu Lissu, kuzuiwa jela na kufunguliwa mashtaka ya uhaini.
Show more...
1 week ago
10 minutes 20 seconds

Wimbi la Siasa
DR Congo: Kabila akutana na wanasiasa wa upinzani jijini Nairobi
Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila, anakutana na wanasiasa wa upinzani jijini Nairobi, kuanzia Oktoba 14,  wiki mbili baada ya kuhukumiwa kifo na Mahakama ya kijeshi. Wanasiasa hao wanazungumza nini ? Tunachambua.
Show more...
3 weeks ago
10 minutes 10 seconds

Wimbi la Siasa
Uchambuzi: Kwanini waasi wa AFC/M23 waendelea kujiimarisha zaidi mashariki mwa DRC ?
Wachambuzi wa mambo wanaona kuwa waasi wa AFC/M 23 wanaendelea kujiimarisha zaidi kisiasa na kiuchumi,  katika maeneo wanayodhibiti, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, licha ya kuwepo kwa mkataba wa Washington uliokubaliwa kati ya DRC na Rwanda kuhusu namna ya kupata mwafaka wa kudumu. Hatua hii inamaanisha nini ? Tunachambua. 
Show more...
4 weeks ago
10 minutes 9 seconds

Wimbi la Siasa
Rais Museveni kuchuana tena na Bobi Wine kwenye uchaguzi wa urais 2026
Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Uganda, uliopangwa kufanyika Januari 12, 2026, zilianza Septemba 29. Kuna wagombea wanane wa urais, akiwemo kiongozi wa muda mrefu Yoweri Museveni mwenye umri wa miaka 81, ambaye ameongoza nchi hiyo kwa miaka 39. Mpinzani wake mkuu ni Robert Kyagulanyi  maarufu kama Bobi Wine, mwenye umri wa miaka 43. Nini kinachotarajiwa kwenye kampeni hizi ?
Show more...
1 month ago
10 minutes 8 seconds

Wimbi la Siasa
DR Congo: Nini hatima ya Kamerhe, baada ya kujiuzulu Uspika ?
Vital Kamerhe, Septemba 22, alijiuzulu kama Spika wa Bunge la taifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya kuundwa kwa Tume ya kumchunguza dhidi ya madai ya matumizi mabaya ya madaraka, kuwahangaisha wabunge na kuwalazimisha kupitisha miswada haraka haraka.Nini hatima ya kisiasa ya Kamerhe baada ya kujiuzulu ? Ataendeleza ushirikiano wake wa karibu na rais Felix Tshisekedi ?
Show more...
1 month ago
10 minutes 7 seconds

Wimbi la Siasa
Nini hatima ya Sudan Kusini baada ya Machar kufunguliwa mashtaka ya uhaini ?
Nchini Sudan Kusini, serikali ya rais Salva Kiir, imetangaza kumfungulia mashtaka ya uhaini na uhalifu wa kivita, kiongozi wa upinzani Riek Machar, ambaye ameondolewa kwenye nafasi ya Makamu wa kwanza wa rais, kufuatia shambulio la wapiganaji wa White Army kwenye kambi ya jeshi katika  jimbo la Upper Nile mwezi Machi mwaka 2025. Nini hatima ya Machar na Sudan Kusini ?
Show more...
1 month ago
10 minutes

Wimbi la Siasa
Kwanini wakaazi wa Uvira hawamtaki Jenerali Olivier Gasita ?
Mji wa Uvira, jimboni Kivu Kusini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa zaidi ya wiki moja, ikiwemo Septemba 08, umeshuhudia maandamano yaliyopangwa na mashirika ya kiraia na wapiganaji wa Wazalendo, kupinga kupinga kuteuliwa kwa Jenerali Olivier Gasita, kuwa Naibu Kamanda wa Kikosi cha jeshi la FARDC, katika eneo hilo kwa madai ya kuwa na ushirikiano na waasi wa AFC/M23 kwa sababu ya kabila lake la Banyamulenge.
Show more...
1 month ago
10 minutes 1 second

Wimbi la Siasa
Tanzania yaingia kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu
Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu kuanzia Agosti 28, kuelekea kufanyika kwa uchaguzi uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025. Rais Samia Suluhu Hassan, kutoka chama tawala CCM, anawania uongozi wa nchi hiyo. Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea  kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.
Show more...
2 months ago
10 minutes

Wimbi la Siasa
Trump atafanikiwa kumaliza vita vya Urusi nchini Ukraine ?
Rais wa Marekani Donald Trump, amechukua hatua ya kuongoza harakati za kumaliza vita vya miaka mitatu vya Urusi nchini Ukraine. Trump amekutana na rais Vladimir Putin na Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine pamoja na viongozi wengine wa nchi za Ulaya  Agosti 18, baada ya awali kukutana na rais Putin Agosti 15 jimboni Alaska. Je, Trump atafanikiwa  kumaliza vita hivyo ?
Show more...
2 months ago
10 minutes

Wimbi la Siasa
Serikali ya DRC na waasi wa M23/AFC wakubaliana kumaliza vita
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M 23/AFC, Julai 19, walitia saini rasimu ya makubaliano jijini Doha nchini Qatar ya namna ya kusitisha vita Mashariki mwa DRC na kupata amani ya kudumu. Ni mambo yepi yaliyokubaliwa na changamoto zipi zinazokabili pande hizi mbili kwenye utekelezwaji ? Tunajadili.
Show more...
3 months ago
10 minutes

Wimbi la Siasa
Rais Museveni ateuliwa tena kuwania urais nchini Uganda
Kiongozi wa muda mrefu nchini Uganda Yoweri Museveni mwenye umri wa miaka 80, ameteuliwa na chama chake cha NRM, kugombea tena urais wakati wa uchaguzi mkuu uliopagwa kufanyika mapema mwaka 2026, baada ya kuwa madarakani miaka 40. Hii inamaanisha nini katika siasa za Uganda ?
Show more...
3 months ago
10 minutes 10 seconds

Wimbi la Siasa
Kwanini vijana wa Gen Z wanaendelea na maandamano nchini Kenya ?
Vijana nchini Kenya maarufu kama Gen Z, wameendelea kuandamana dhidi ya serikali ya rais William Ruto. Maandamano haya yameishia kwenye maafa na majeruhi tangu mwezi Juni mwaka 2024. Tunaungana na wanafunzi wa chuo cha ufundi cha NIBS kilichopo Ruiru, kusikia kutoka kwao. Kwanini wanaandamana ?
Show more...
4 months ago
10 minutes 29 seconds

Wimbi la Siasa
Je, mkataba kati ya DRC na Rwanda utaleta amani ya kudumu ?
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda, walitia saini mkataba wa amani, chini ya uangalizi wa Marekani, Juni Juni 27 2025, jijini Washington DC, unaolenga kurejesha amani ya kudumu Mashariki mwa DRC. Nchi hizo mbili zimekubaliana kushirikiana kuyaondoa makundi yenye silaha. Mkataba huu umepokelewa vipi nchini DRC ?
Show more...
4 months ago
10 minutes 19 seconds

Wimbi la Siasa
Je, usitishwaji wa vita kati ya Israel na Iran utadumu ?
Israel na Iran zimekubali pendekezo la rais wa Marekani Donald Trump, kuacha kushambuliana baada ya vita vya siku 12 vilivyosababisha vifo zaidi ya 600 nchini Iran na zaidi ya 20 nchini Israeli. Israeli ilianza mashambulio hayo, kwa kulenga vituo vya  nyuklia vya Iran  kwa lengo la kuizuia kutengeneza silaha za maangamizi. Je, usitishwaji huu wa vita utadumu ?
Show more...
4 months ago
10 minutes 1 second

Wimbi la Siasa
Nini kipo nyuma ya mkataba wa ushirikiano kati ya Kenya na Falme za Kiarabu ?
Serikali ya Kenya mwezi Januari 2025, ilisaini mkataba wa ushirikiano wa kibiashara na nchi ya Falme za Kiarabu kukuza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Mswada huo umezua pingamizi kubwa kutoka kwa wanaharakati, watunga será na wapinzani wa serikali na wanataka wabunge kuufanyia marekebisho.
Show more...
4 months ago
10 minutes

Wimbi la Siasa
Trump azuia raia wa nchi 12 kuzuru Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ameagiza raia wa nchi 12 hasa kutoka Afrika kutozuru nchi hiyo. Agizo hilo lilianza kutekelezwa Juni 9, 2025. Trump anasema amechukua hatua hii kwa sababu za kiusalama. Wakati hayo yakijiri, maandamano yamekuwa yakishuhudiwa katika mji wa Los Angeles, kupinga sera ya Trump ya kuwasaka na kuwafukuza nchini humo, wageni wanaoishi bila vibali. Tunachambua kwa kina.
Show more...
4 months ago
10 minutes 10 seconds

Wimbi la Siasa
Sudan yampata Waziri Mkuu, vita vikiendelea kupamba moto
Uongozi wa kijeshi nchini Sudan mwishoni mwa mwezi Mei, ulimteua mwanasiasa  na mwanadiplomasia mkongwe Kamil Idris, kuwa Waziri Mkuu mpya wakati huu vita vikiendelea kati ya jeshi na wanamgambo wa RSF. Tangu kuanza kwa vita Aprili 2023, watu zaidi ya 20,000 wamepoteza maisha, huku wengine Milioni 15 wakikimbia makaazi yao, wakiwemo zaidi ya Milioni nne ambao wamekimbilia katika nchi jirani kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa. Nini hatima ya Sudan ?
Show more...
5 months ago
10 minutes 26 seconds

Wimbi la Siasa
DR Congo: Kabila aondolewa kinga ya kutoshtakiwa, aripotiwa kufikia Goma
Maseneta nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wamemwondolea kinga ya kutoshtakiwa  rais wa zamani Joseph Kabila , ambaye ripoti zinasema alirejea Goma usiku wa Mei 25.Kiongozi huyo wa zamani, ameishtumu serikali ya rais Felix Tshisekedi na kuuita ya  Kidikteta. Hata hivyo, serikali ambayo inamtuhumu kiongozi huyo wa zamani kwa kushirikiana na waasi wa M23.
Show more...
5 months ago
10 minutes 9 seconds

Wimbi la Siasa
Wanaharakati kutoka Kenya wafukuzwa nchini Tanzania
Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu na Mawakili mashuhuri kutoka nchini Kenya, akiwemo Martha Karua na Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga, walifukuzwa nchini Tanzania, Mei 19, walikokuwa wamekwenda kama mashuhuda wa kesi ya uhaini inayomkabili kiongozi wa upinzani Tundu Lissu.  Rais Samia Suluhu Hassan ameonya kuwa nchi yake haitaruhusu wanaharakati kutoka nje, kuvunja amani ya nchi yake. Tunachambua kilichotokea nchini Tanzania.
Show more...
5 months ago
10 minutes

Wimbi la Siasa

Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa