
Uchambuzi Wa Kitabu Cha Biblia ni kipindi kinachokuwezesha kulijua Neno la Mungu kwa undani na kwa kina zaidi ili kumfahamu Mungu na mapenzi yake kupitia maandiko mbalimbali tunayokuwa tukiyapitia katika Biblia nzima. Tunachambua Biblia kitabu kwa kitabu, sura kwa sura na neno kwa neno ili msikilizaji aweze kuelewa mazingira neno lilipozungumziwa na kuelewa taafsiri ya neno husika kwa muktadha uliotumika. Kila andiko tulisomalo katika Biblia tunalitafsiri kwa mujibu wa agano jipya ili tuweze kutembea katika Neno la Mungu kwa wakati tulionao. Msikilizaji anaweza kutumia ufunuo anaoupata kwenye vipindi hivi na kuutumia katika eneo lolote la maisha yake mfano katika kazi zake za kila siku, katika ndoa/familia na katika huduma mtu aliyonayo.