
Wakati baadhi ya Watanzania wakila na kusaza kiasi cha kutupa chakula, ripoti mpya ya usalama wa chakula na lishe Tanzania inakadiria kuwa kuanzia Mei 2022 watu 592,000 watakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na kushuka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo nchini.
Ripoti hiyo ya Tathmini ya Usalama wa Chakula na Lishe iliyotolewa Februari 2022 na Wizara ya Kilimo na Idara ya Udhibiti Maafa ya Ofisi ya Waziri Mkuu imeeleza kuwa hali hiyo ya uhaba mkubwa wa chakula itashudiwa kati ya mwezi Mei hadi Septemba mwaka huu.
Nini sababu? Herimina Mkude anasimulia zaidi.