Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Society & Culture
Business
News
Sports
TV & Film
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts125/v4/0e/44/af/0e44af17-fc29-ac16-6ba9-db2bf25c4dca/mza_12684382132760653712.jpg/600x600bb.jpg
Nukta the Podcast
Nukta Habari
71 episodes
1 week ago
Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.
Show more...
Entertainment News
News
RSS
All content for Nukta the Podcast is the property of Nukta Habari and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.
Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.
Show more...
Entertainment News
News
https://d3t3ozftmdmh3i.cloudfront.net/staging/podcast_uploaded_episode/16079322/16079322-1696082827954-9f2c5e2edd22.jpg
UPUNGUFU WA WALIMU SHULE YA MSINGI UNAVYOATHIRI ELIMU TANZANIA
Nukta the Podcast
9 minutes 34 seconds
2 years ago
UPUNGUFU WA WALIMU SHULE YA MSINGI UNAVYOATHIRI ELIMU TANZANIA

Wakati watahiniwa zaidi ya milioni moja wa elimu ya msingi Tanzania Bara wakiwa wanasubiri hatma yao, baada ya kumaliza mitihani yao jana Septemba 14, 2023, utoshelevu wa walimu katika ngazi hiyo muhimu ya elimu kwa shule za Serikali umeendelea kuwa kitendawili

Kitabu cha hali ya uchumi cha mwaka 2022, kinabainisha kuwa mpaka Disemba mwaka 2022 kulikuwa na jumla ya wanafunzi milioni 10.8 katika shule za msingi za Serikali Tanzania, huku idadi ya walimu katika shule za Serikali ikiwa 173,276.

Hii ni sawa na kusema idadi ya wanafunzi waliopo ni mara 62 zaidi ya idadi ya walimu na hivyo kwa wastani mwalimu mmoja hufundisha darasa lenye wanafunzi 63 kwa wakati mmoja uwiano ambao uko juu ya kiwango kinachotakiwa cha wanafunzi 45 kwa darasa.

Aidha, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) inataja Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma kuwa ndio wilaya ambayo mwalimu mmoja hufundisha darasa lenye wanafunzi wengi zaidi wanaofika 103.

Wilaya ya Muleba iliyopo mkoani Kagera ndiyo wilaya pekee iliyofanikiwa kufikia uwiano stahiki kwa wanafunzi 45 kufundishwa na mwalimu mmoja kwa darasa mwaka 2021.

Wadau wa elimu nchini Tanzania, wanatoa maoni yao juu ya namna upungufu wa walimu shule za msingi unavyoathiri sekta ya elimu nchini.

Karibu.

Nukta the Podcast
Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.