Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Society & Culture
Music
History
News
Business
Education
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts125/v4/0e/44/af/0e44af17-fc29-ac16-6ba9-db2bf25c4dca/mza_12684382132760653712.jpg/600x600bb.jpg
Nukta the Podcast
Nukta Habari
71 episodes
6 days ago
Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.
Show more...
Entertainment News
News
RSS
All content for Nukta the Podcast is the property of Nukta Habari and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.
Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.
Show more...
Entertainment News
News
https://d3t3ozftmdmh3i.cloudfront.net/staging/podcast_uploaded_episode/16079322/16079322-1692338707780-513e3bdf0c8d7.jpg
Teknolojia ya vifuu vya nazi itakavyo waokoa wachimbaji na madhara ya zebaki
Nukta the Podcast
7 minutes 7 seconds
2 years ago
Teknolojia ya vifuu vya nazi itakavyo waokoa wachimbaji na madhara ya zebaki

Huenda wachimbaji wadogo wa madini Tanzania wakaepukana na athari za afya pamoja na uchafuzi wa mazingira ikiwa wataasili matumizi ya bidhaa mpya ya kusafishia madini (Activated carbon) inayozalishwa nchini.

Bidhaa hiyo inayotengenezwa kwa kutumia vifuu vya nazi itachochea uzalishaji wa madini na kuongeza mchango wa sekta hiyo kwenye pato la taifa  kwa kuwa itapatikana kwa urahisi jambo litakaloongeza kasi katika shughuli za uchenjuaji huku mazingira na wachimbaji wakwa salama.

Upatikanaji wa bidhaa hiyo mbadala wa zebaki katika shughuli za uchechuaji itakuwa mkombozi kwa wachimbaji pamoja na jamii ambayo inaweza kuathirika kwa kwa kuvuta hewa, kula chakula au maji yaliyo na sumu ya zebaki.

Shirika la Afya Duniani (WHO), linabainisha kuwa athari za kiafya zitokanazo na zebaki ni pamoja na kuharibiwa kwa mifumo ya neva, kuharibiwa kwa mfumo wa upumuaji, mmeng’enyo, mifumo ya kinga, figo, mapafu na wakati mwingine husababisha kifo.

WHO wamesisitiza kuwa sumu hiyo inaweza kusababisha magonjwa katika mfumo wa fahamu ikiwemo kifafa, kupoteza uwezo wa kuona au kusikia, udumavu pamoja na kupoteza kumbukumbu

Mpango Kazi wa Taifa wa Kupunguza Matumizi ya Zebaki 2020/25 unabainisha kuwa zebaki ni miongoni mwa kemikali hatarishi inayosababisha athari kwa afya ya binadamu na mazingira duniani

Nukta the Podcast
Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.