
Ziwa Victoria ni moja ya maziwa makuu ya Afrika Mashariki. Ni ziwa ambalo lipo kwenye mstari wa ikweta na limezungukwa na nchi tatu zilizopo Afrika Mashariki yaani Tanzania, Kenya na Uganda.
Ziwa hili ni chanzo cha Mto Nile wenye urefu wa kilomita 6,650 na urefu huo unaufanya kuwa mto mrefu zaidi duniani, Ziwa Victoria ndiyo ziwa kubwa zaidi barani Afrika na lina ukubwa wa kilomita za mraba 68,800 ambapo ni la pili duniani kwa ukubwa likitanguliwa na Ziwa Superior lililopo Amerika ya kaskazini, kwa ukubwa huu nchi za Rwanda na Burundi zinaweza kuwa visiwa ndani ya ziwa hili.
Ziwa hili linahudumia wakazi takribani milioni 40 wa Afrika Mashariki kupitia shughuli za uvuvi, utalii na usafirishaji ambazo hufanyika kila siku, miongoni mwa wanaotegemea ziwa hili katika shughuli zao za kila siku ni Mwajuma Chamuriho, mwanamama huyu amejiajiri na ametengeneza ajira zaidi ya 50 owa watu wengine kupitiz Ziwa Victoria.
lakini Mwajuma ni nani hasa, nini kilimsukuma kuwekeza katika uvuvi kazi ambayo inatafsiriwa kuwa nya wanaume zaidi, fuatana na Abdulshakur katika makala hii ya dakika saba, natumai utajifunza mengi.