
Mara nyingine tunakuwa na imani ya kuanza kitu au kupokea uponyaji lakini baada ya muda kidogo uponyaji unapeperuka au kile tulichokianza kinakwama. Tunakuwa kama Petro ambaye alianza kutembea juu ya maji halafu akaona upepo mkali akaogopa na kuanza kuzama. Tunaacha kuangalia chanzo cha imani yetu, yaani Kristo Yesu, na kuangalia mazingira. Kumbuka mwenye haki ataishi kwa imani si kwa kuona.