
Tumepewa mamlaka ya kukanyaga simba na nyoka, naam, mwanasimba na joka tunapaswa kuwaseta kwa miguu. Ukifuatilia hili "joka" ambalo Mkristo umepewa mamlaka ya kulikanyaga utafahamu kwamba ni lile joka, yaani Shetani au Ibilisi kwa jina. Kwa mamlaka uliyonayo siyo tu kwa vibaraka wa shetani bali hata kwa shetani mwenyewe. Ndiyo maana maandiko yanasema mpingeni Shetani naye atawakimbia. Kama baba yao anawakimbia itakuwaje kwa wanae, yaani wachawi!? Kama umeokoka na unajua mamlaka na nguvu ulizonazo, wewe ni tishio kwa nguvu za giza. Sikiliza somo hili fupi ukawafundishe na wengine.