
Biblia inatuonyesha namna ambavyo Bwana Mungu anataka watu wake wawe hodari katika kufanya yale aliyowaamuru wayafanye; hakuna haja ya kuogopa kwa sababu Roho Yake ipo kati ya watu Wake.
Kama wewe ni mwaminini basi huna haja ya kuogopa kwa sababu yale aliyosema nao wakati ule bado yanakuhusu wewe hata leo hii kwa sababu kama mwamini bado Roho Mtakatifu yuko ndani yako. Ukiwa hodari kufanya kazi ya Bwana ndipo utaona utukufu wa mwisho unakuwa mkuu kuliko utukufu wa kwanza.
Sikiliza fundisho hili, utaimarika.