
Kutoogopa ni suala la imani kwa sababu inakupasa kusimama na maandiko kwa imani kwamba yuko Mungu anayakuzungukia pande zote na tena anayeangalia kwamba ufikie mwisho mwema. Na pia kwa sababu woga ni udhihirisho wa kutoamini au kuwa na imani haba hivyo haikwepeki kwamba mambo yanayoathiri imani yako yanagusa moja kwa moja kuogopa au kutoogopa kwako. Katika episode hii tunaangalia mambo manne yanayoathiri imani ili kukuwezesha kuikuza imani yako uweze kuwa jasiri, usiyeogopa, kwa sababu Biblia inasema usiogope.