
Katika maisha ya imani Shetani hupigana vita ili kututoa katika ujasiri tulionao katika Kristo Yesu. Na adui hufanikiwa katika hili pale anapoweza kutujaza dhamiri ya hatia ndani yetu kwamba sisi ni wakosa na hatuna haki mbele za Mungu. Wakristo wengi wanaishi katika dhamiri ya hatia au wataingia kwenye huo mtego hivi karibuni kwa sababu wameshapelekwa kwenye kona ya kuamini kwamba haki yao inatokana na matendo yao mazuri, yaani hawajavunja sheria au torati. Haki yetu haitokani na sheria bali imani na tena tunalo ondoleo la dhambi. Hati iliyokuwa na mashtaka dhidi yako iligongomewa msalabani pale alipokufa Mwokozi wa ulimwengu. Huna hatia! Sikiliza somo hili.