
Katika episode hii ya 5 tunajadili mada inayogusa maisha ya wengi: Kubadilisha Makazi au Nchi – Je, Kunaweza Kuleta Maendeleo Binafsi? Jackson Lusagalika na Kefa Victor wanaangazia faida, changamoto, na mbinu za kufanikiwa unapochukua hatua ya kuhamia nchi au makazi mapya.
Tutashuhudia mifano hai ya watu maarufu kama Elon Musk, Lupita Nyong’o, na Chimamanda Ngozi Adichie, ambao walifanikiwa kutumia fursa za kubadilisha nchi kuendeleza ndoto zao. Pia, changamoto kama utambulisho wa kitamaduni, umbali na familia, na changamoto za kisheria zinajadiliwa kwa kina.