Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Society & Culture
Business
Sports
History
Fiction
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts125/v4/b6/98/71/b6987197-c8a0-7dbc-c186-f102da2d49af/mza_11831379832986323838.jpg/600x600bb.jpg
St. Joseph Cafasso King'ong'o Parish
St Joseph Cafasso King'ong'o Parish
17 episodes
2 days ago
Joseph Cafasso (Italian: Giuseppe Cafasso; 15 January 1811 – 23 June 1860) was an Italian Roman Catholic priest who was a significant social reformer in Turin. He was one of the so-called "Social Saints" who emerged during that particular era. He is known as the "Priest of the Gallows" due to his extensive work with those prisoners who were condemned to death. But he was also known for his excessive mortifications despite his frail constitution: he neglected certain foods and conditions to remain as frugal and basic as possible unless a doctor ordered otherwise. King'ong'o Catholic Parish
Show more...
Christianity
Religion & Spirituality
RSS
All content for St. Joseph Cafasso King'ong'o Parish is the property of St Joseph Cafasso King'ong'o Parish and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.
Joseph Cafasso (Italian: Giuseppe Cafasso; 15 January 1811 – 23 June 1860) was an Italian Roman Catholic priest who was a significant social reformer in Turin. He was one of the so-called "Social Saints" who emerged during that particular era. He is known as the "Priest of the Gallows" due to his extensive work with those prisoners who were condemned to death. But he was also known for his excessive mortifications despite his frail constitution: he neglected certain foods and conditions to remain as frugal and basic as possible unless a doctor ordered otherwise. King'ong'o Catholic Parish
Show more...
Christianity
Religion & Spirituality
https://d3t3ozftmdmh3i.cloudfront.net/production/podcast_uploaded/4053789/4053789-1585143807335-081cbeed8fa2f.jpg
Wednesday 25 2020 Daily Mass
St. Joseph Cafasso King'ong'o Parish
34 minutes 24 seconds
5 years ago
Wednesday 25 2020 Daily Mass

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2020
JUMATANO, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SHEREHE YA KUPASHWA HABARI YA KUZALIWA BWANA

SOMO 1
Isa. 7:10 – 14

Bwana alisema na Ahazi akinena,  Jitakie ishara ya Bwana, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini  sana, au katika mahali palipo juu sana. Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka,  wala sitamjaribu Bwana. Naye akasema, Sikilizeni sana, enyi nyumba ya  Daudi; Je! Ni neno dogo kwenu kuwachosha wanadamu, hata mkataka  kumchosha Mungu wangu pia? Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara.  Tazama, Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita  jina lake Imanueli.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 40:6 – 10 (K) 7 , 8

(K) Tazama, nimekuja, Ee Bwana, kuyafanya mapenzi yako.

Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua,
Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja. (K)

Katika gombo la chuo nimeandikiwa
Kuyafanya mapenzi yako,
Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;
Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. (K)

Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa,
Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua. (K)

Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;
Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Sikuficha fadhili zako wala kweli yako
Katika kusanyiko kubwa. (K)

SOMO 2
Ebr. 10:4 – 10

Haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. Kwa hiyo ajapo  ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea  tayari; Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo;  Ndipo niliposema, Tazama nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa)  niyafanye mapenzi yako, Mungu.
Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo  na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa  nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati), ndipo aliposema, Tazama,  nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi  alisimamishe la pili. Katika mapenzi hayo tumepata utakaso, kwa kutolewa  mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Yn. 1:14

Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukaona utukufu wake.

INJILI
Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa  Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa  na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni  Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema.  Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake,  akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia,  Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua  mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa  mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye ju, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi  cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme  wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno  hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu  atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli;  kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa  Mungu. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto  mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa  tasa; kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akasema,  Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha  malaika akaondoka akaenda zake.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

St. Joseph Cafasso King'ong'o Parish
Joseph Cafasso (Italian: Giuseppe Cafasso; 15 January 1811 – 23 June 1860) was an Italian Roman Catholic priest who was a significant social reformer in Turin. He was one of the so-called "Social Saints" who emerged during that particular era. He is known as the "Priest of the Gallows" due to his extensive work with those prisoners who were condemned to death. But he was also known for his excessive mortifications despite his frail constitution: he neglected certain foods and conditions to remain as frugal and basic as possible unless a doctor ordered otherwise. King'ong'o Catholic Parish