Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Society & Culture
Business
Sports
TV & Film
Health & Fitness
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts115/v4/96/f3/75/96f375be-cda2-e83c-df72-2c8843220004/mza_11164014232092982709.jpg/600x600bb.jpg
Iran-Tanzania Podcast
Iran.Tanzania
12 episodes
1 week ago
Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Show more...
Society & Culture
RSS
All content for Iran-Tanzania Podcast is the property of Iran.Tanzania and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.
Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Show more...
Society & Culture
https://d3t3ozftmdmh3i.cloudfront.net/production/podcast_uploaded_episode400/15301747/15301747-1647002815546-b0f0700d895ed.jpg
Mwanamalenga wa Kiirani Nezami
Iran-Tanzania Podcast
12 minutes 36 seconds
3 years ago
Mwanamalenga wa Kiirani Nezami

Jamaluddin Abu Mohammad hakuweza kupata upendo wa wazazi  wake kwa muda mrefu; kwani wazazi wake walifariki dunia  akiwa  bado mtoto na kupata malezi akiwa mtoto yatima. Ushahidi wa kihistoria unaonyesha kuwa, Nezami Ganjavi hakuwahi kuondoka katika mji wa Ganja akiwa bado na umri mdogo, na alipofikia marika ya ujana , aliweza kujifunza sanaa na ujuzi  mbalimbali na hatimaye alikuwa na ufasaha wa kuzungumza na kuandika lugha za Kiazeri, Kiarabu, Kiajemi na Kipahlavi.

Nezami ni bingwa na mshairi anayepaswa  kuzingatiwa kwenye mihimili na nguzo za ushairi wa Kiajemi. Yeye ni mmoja wa malenga aliyekuwa na kipaji cha kuandika mashairi na kuyasoma kwa sauti nzuri, iliyowavutia wasikilizaji. Ingawa hekaya na simulizi za hadithi za Kiajemi hazikuanzishwa na Nezami, lakini  gwiji huyo anahesabiwa kuwa ni mshairi pekee  aliyeweza kuendeleza ushairi wa mafumbo  kwa  kiwango cha juu zaidi kufikia mwisho wa karne ya sita.

Nezami aliweza kujiwekea nafasi maalumu katika fasihi ya lugha ya Kifarsi inayotumika  Iran na ametumia takriban miaka thelathini ya maisha yake akitunga mkusanyiko wake wa mashairi yanayoitwa "Hazina Tano" au "Khamseh". Mkusanyiko huu una mashairi matano marefu, ambayo ni: "Makhzan al-Asrar", "Khosrow na Shirin", "Lalya na Majnoon", "Haft Peykar" na "Iskander Nameh" ni hazina tano. Pia, mkusanyo wa mashairi yaliyosalia kutoka kwa Nezami ni pamoja na mashairi, mashairi ya sauti vipande ambavyo vina nafasi maalumu katika fasihi ya Kiajemi.

Ingawa umaarufu mwingi wa Nezami unatokana na kutunga mashairi ya mapenzi, yenye hekima na sahili. Kwa maneno mengine, mashairi yake ni rahisi lakini ya kina, na mashairi yake yalikuwa yanamfanya mtu kufikiria na kutafakari kwa kina ili kupata siri iliyofichwa katika maneno yake. Kuna jumbe nyingi za kifalsafa ambazo zimeelezwa kwa kutumia maneno mepesi  na fasaha,  badala ya kutumia maneno magumu na mazito. Nyingi za beti zake za mashairi zilikuwa zikielezea  maisha ya akhera, sanjari na kuyafurahia maisha mafupi ya ulimwenguni. 

Kuna tofauti za maoni kuhusu kuzaliwa kwa baba wa mshairi Nezami Ganjavi, na baadhi ya vyanzo vinaeleza kuwa anatoka Tafresh au Farahan. Lakini Behrouz Thorotian (mtafiti wa fasihi, mwanasayansi na profesa mstaafu) anaeleza kuwa,  mwanzo wa beti za mashairi ya Layla na Majnoon, zinaonyesha kuwa alikuwa na asili ya Kiajemi. Ameendelea kusema kuwa, ubeti wa 36 wa shairi la Leyla  na Majnoon, unafichua kazi na nafasi ya mshairi ambaye alikuwa Dehqan yaani “mkulima” na kuitambulisha jamii yake kuwa ni  Muajemi.

Kwa Wairani neno Dehqan "mkulima" linamaanisha  mmiliki wa ardhi ya kilimo;  malenga  Ferdowsi naye katika beti zake amefafanua kuwa,  tafsiri ya neno hilo  lilitumika baadaye kwa Wairani wote. Kwa kuongezea, neno Dehqan "mkulima" lilitumiwa pia kwa maana ya  "mwanahistoria". Kwa hivyo, inaweza kueleweka kuwa Nezami  Ganjavi anajitambulisha kama malenga, mkulima wa Iran, mwanahistoria, muimbaji wa mashairi  na mmiliki wa ardhi ya kilimo. Wakulima wamekuwa na jukumu la kuhifadhi tamaduni na historia ya Iran katika kipindi cha Kiislamu, na kwa ufupi, familia ya Nezami Ganjavi inaweza kuchukuliwa kuwa familia ya wakulima wenye ufahamu wa kitamaduni na utajiri wa mali ambao wamekuwa na nafasi muhimu katika fasihi.

Nezami Ganjavi alikuwa mshairi mashuhuri, mwandishi wa riwaya, mwenye hekima na ambaye amekuwa  na ushawishi mkubwa katika fasihi ya Kiajemi na daima ametajwa kuwa mtu muhimu katika historia.

Dola la Uajemi ni moja kati ya madola makubwa yaliyokuwa yakitawala duniani. Jamhuri ya Azerbaijan, iliyoko katika eneo la Caucasia kati ya Ulaya na Asia ilikuwa chini ya himaya ya dola la Uajemi katika zama hizo. 


Iran-Tanzania Podcast
Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran